Saturday, February 9, 2013

Hatimaye Wanawake Mashujaa Tanzania imezinduliwa rasmi leo mkoani Singida!

Wapendwa Wanaharakati wa wanawake mashujaa Tanzania, napenda kuwahabarisha kuwa Taasisi yetu imesajiliwa leo rasmi kama Taasisi inayosaidiana na Jamii na Serikali ili kuweza kutengeneza jamii imara katika nyanja ya familia na malezi ya watoto.

Tunamshukuru Mh. Manju Salum Msambya Mkuu wa Wilaya ya Ikungi kwa kujali na kuja kufungua kongamano letu la ufunguzi wa Kongamano la Wachumba na Wanandoa ili kuweza kufanya shughuli zake rasmi hapa Singida na nje ya Singida.

Tunamshukuru Mkuu wa Mkoa wa Singida Dct. Parseko Vincent Korne, kwa kujali mualiko wetu na kuweza kutupa Mgeni Rsmi anaye muamini na kumtambua kazi yake vizuri ili kuwa mgeni raasmi, Napenda kutoa shukurani kwa serikali, Mshauri mkuu wa Taasisi ya Wanawake Mashujaa Tanzania ndugu, Selestine Onditi (DAS) SINGIDA. Kwa mchango wake mkubwa alioonesha hadi kufanikisha ufunguzi huu.

Nawashukuru wadau wote na washiriki wote waliojali na kuchangia kwa hali na mali katika kushiriki kongamano la wapendanao, tuna amini huu ni mwanzo mzuri na ushindi ni mkubwa.

Sitaacha kumshukuru MC wangu maarufu na mashuhuri kutoka Arusha, Mc Rosse Mosha aka PRETTY LADY Mungu ambariki sana na endapo utakuwa unahitaji shughuli yoyote ya kitchen party, sendoff, harusi n.k usisite kumtafuta! +255 767233323/255789647694

No comments:

Post a Comment