Friday, January 18, 2013

INAPENDEZA SANA KULA CHAKULA PAMOJA NA FAMILIA YAKO

Nawasalimu sana wapendwa wangu, leo napenda kuzungumzia jinsi mfumo wa kula pamoja na familia yako unavyoweza kukusaidia katika kuijuwa familia yako vizuri, tukianza na mama, baba na watoto pia ni vyema kama kuna kijana/ binti wa kazi awepo pia katika meza ya chakula.

Faida ambazo mtazipata zitafanana na hizi endapo mtasimama katika jambo hili ipasavyo.
  • Kufahamu usalama wa wale unaowahudumia hapo ndani, nikimaanisha kuwa mkila pamoja mezani mtaweza kuhakiki nani yupo mezani na nani hayupo mezani  na ni kwa nini?
  • Pili mtaweza kufahamu ambaye hayupo ana tatizo gani, au ni mgonjwa au ni mjamzito n.k
  • Tatu mtakapo maliza kula mnaweza kujadili mambo mbali mbali yahusuyo familia yako ukiwa kama baba na mama, mtaweza kusikiliza maoni ya watoto wenu kuhusu mwenendo mzima wa familia na wanavyoishi shuleni na katika jamii iliyowazunguka.  
HASARA
  • Hasara zinazoweza kutokea ni kutojuwa familia yako kwa undani, hii inatokana na kutokuwa na ratiba nzuri juu ya familia yako.
  • Watoto wako na jamii yako vitaweza kupotea kutokana na kutokuwa na ulinzi mzuri kiasi cha kwamba mwisho wa siku unajutia uzazi wako.
  • Mabinti zetu wanabeba mimba na hata wazazi/walezi hawajui chochote hadi anakuja kukuta mtoto anakaribia kujifungua ndo mzazi anashtuka.
  • Kutofahamu hali ya maisha wanayoishi wanafamilia yako, n.k

No comments:

Post a Comment