Friday, January 18, 2013

NDUGU MZAZI/MLEZI UNAFAHAMU KIJANA WAKO ANA MARAFIKI WA AINA GANI?





Vijana wengi walio na malezi mazuri huwa waoga sana kujiingiza katika makundi ya watoto wenye malezi mabaya, hii ni kutokana na uangalizi wa wazazi/walezi.

Tunafanyaje katika jambo hili? Wengi wetu tumekuwa bize sana na kazi na biashara kuliko kusimamia swala zima la malezi. Watoto wetu wamekuwa wakivutwa na makundi mabaya sana kutokana na upweke walionao nyumbani, kwani wanakosa watu wa kuwasaidia kimawazo na kuwafundisha watoto wao jinsi ya kujisaidia kimawazo.

Tusifanye kazi sana hadi kusahau watoto wetu, hawa ndio wanaotufanya sisi tushindwe kukaa nyumbani na kuahangaikia, sasa endapo tutawasahau itakuwa haina maana kabisa kwani mwisho wa siku hakuna maana yoyote ya kuhangaika.

Suluhu ni nini?

Hakikisha una ratiba ya kudumu kwa ajili ya watoto na familia kwa ujumla ili kutengeneza mambo mazuri kwa familia yako, ukipanga ratiba zako utaweza kujua binti / kijana wako anachojifunza katika marafiki zake na endapo utaona marafiki zake ni wale wenye maadili mabaya basi utaweza kumsaidia kabla hajaharibika zaidi.

No comments:

Post a Comment